a Hes 33:8; Yos 24:6; Isa 43:16; 63:11; 1Kor 10:1; Kut 3:12; 15:19; Kum 31:6-8; Yos 3:16; 4:22; Neh 9:11; Za 66:6; 77:19; 106:9; Isa 11:15; 41:10; 43:5; 44:27; Isa 50:2; 51:10; 63:13; Yer 46:28; Nah 1:4; Ebr 11:29; Kut 15:8; Yos 3:13
Exodus 14:22-27
22 anao Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, maji yakiwa ukuta upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto. 23Wamisri wakawafuatia ndani ya bahari, pamoja na farasi wote wa Farao, magari ya vita na wapanda farasi. 24 bKaribia mapambazuko, Bwana akaliangalia jeshi la Wamisri kutoka ile nguzo ya moto na ya wingu, akalifadhaisha. 25 cMungu akayaondoa magurudumu ya magari yao, kwa hivyo wakayaendesha kwa shida. Nao Wamisri wakasema, “Tuachane na Waisraeli! Bwana anawapigania dhidi ya Misri.”Wafuatiaji Wazama
26Ndipo Bwana akamwambia Musa, “Nyoosha mkono wako juu ya bahari ili maji yarudiane yawafunike Wamisri, magari yao ya vita na wapanda farasi wao.” 27 dMusa akanyoosha mkono wake juu ya bahari, wakati wa mapambazuko bahari ikarudiana na kuwa kama kawaida. Wamisri wakajaribu kuyakimbia maji, lakini Bwana akawasukumia ndani ya bahari.
Copyright information for
SwhKC